_,_._,___
cha mkufuu mwanafuu hu, akila ha na cha mwanafuu mkufuu ha akila hu
Thursday, February 17, 2011
Thursday, February 10, 2011
Laazizi
- Mapenzi kitu ajabu, yakutia bumbuwazi
Yakufanya uwe bubu, kujibu huwa huwezi
Shubiri kwako zabibu, na vitamu huviwezi. - Wamkuta kaemewa, asemayo hayajuwi
Aumba akiumbuwa, aona maruwiruwi
Vigumu kumuopowa, na kwa ngisi kumvuwi. - Hukumbuka ya zamani, yote walofanyiana
Nyumbani barabarani, ayaona kama jana
Akili yake ya nyani, aruka inagongana. - Wangoja nyota ya jaha, kutwa wewe unahaha
Mawazo yako silaha, akukwaaye usaha
Usifanyiwe msaha, waugeuza karaha. - Kalelewa kaleleka, utani kwake ni mwiko
Njiani yeye na kaka, hapokei mualiko
Ghadhabu zake za paka, hapendi maziko.
Aushi ya bin-a-dam
Maisha ya binadamu ni kitu ambacho hakijatiliwa maanani abadan katan. Insi wengi ulimwenguni wanachukulia jambo hili kama sadfa tu. Sie sote twaishi kwa aushi ya kuomba. kuna mambo mengi sana ambayo yanamfinyilia mwanadamu chini. Baadhi yao ikiwa:
1. Pesa.
2.Mume ama mke.
3.Vijulanga.
1. Pesa.
2.Mume ama mke.
3.Vijulanga.
Subscribe to:
Posts (Atom)