Thursday, February 17, 2011

Three Secrets to Happiness



 
 
 
 
 
 
 
_,_._,___

Thursday, February 10, 2011

Laazizi

  1. Mapenzi kitu ajabu, yakutia bumbuwazi
    Yakufanya uwe bubu, kujibu huwa huwezi
    Shubiri kwako zabibu, na vitamu huviwezi.
  2. Wamkuta kaemewa, asemayo hayajuwi
    Aumba akiumbuwa, aona maruwiruwi
    Vigumu kumuopowa, na kwa ngisi kumvuwi.
  3. Hukumbuka ya zamani, yote walofanyiana
    Nyumbani barabarani, ayaona kama jana
    Akili yake ya nyani, aruka inagongana.
  4. Wangoja nyota ya jaha, kutwa wewe unahaha
    Mawazo yako silaha, akukwaaye usaha
    Usifanyiwe msaha, waugeuza karaha.
  5. Kalelewa kaleleka, utani kwake ni mwiko
    Njiani yeye na kaka, hapokei mualiko
    Ghadhabu zake za paka, hapendi maziko.
Hashil S. Hashil

Aushi ya bin-a-dam

Maisha ya binadamu ni kitu ambacho hakijatiliwa maanani abadan katan. Insi wengi ulimwenguni wanachukulia jambo hili kama sadfa tu. Sie sote twaishi kwa aushi ya kuomba. kuna mambo mengi sana ambayo yanamfinyilia mwanadamu chini. Baadhi yao ikiwa:
1. Pesa.
2.Mume ama mke.
3.Vijulanga.